Hymns and Prayers

DAMU IMEBUBUJIKA

1. Damu Imebubujika, ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, husafiwa kweli.

2. Ilimpa kushukuru mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, yanisafi ndani.

3. Kondoo wa kuuawa, damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa, kwa utimilivu.

4. Bwana tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako; taimba milele.

5. Nikifa tazidi kwimba sifa za wokovu
Ulimi ujaponyamaa vumbini mwa ufu.

6. Bwana, umenikirimu nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu ya mali ya kweli.

7. Nikubali kukwimbia, mbinguni milele,
Mungu nitakusifia Jina lako pweke.

  • Hymn
  • 8,912 views